Leo ZIFF tunalia, katuondoka Jasiri.
Alikuwa jasiri wa mawazo na udiriki,
Msema kweli asiyeogopa kuchukiwa,
Mwoga wa aibu ya ukimya wa woga.
Alikuwa kijinga cha moto kiwashao msitu,
Mparamia mnazi si kwa mnazi ila nazi,
Mpishi wa chakula cha wanaharakati,
Akashika tama kwa kuona aibu ya mvivu.
.